Leo tarehe 5 Novemba 2025 – Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Tanzania (NECTA), Profesa Said A. Mohamed, ametangaza matokeo ya Mtihani wa Kumaliza Elimu ya Msingi (darasa la saba) kwa mwaka 2025. Tangazo hilo limefanyika leo jijini Dar es Salaam huku matokeo yakionyesha mafanikio makubwa kwa wanafunzi wa darasa la saba nchini Tanzania.
Kwa mujibu wa taarifa rasmi zilizotolewa, jumla ya watahiniwa 937,581, sawa na asilimia 81.80 ya watahiniwa 1,146,164 waliopata matokeo, wamefanikiwa kuipita mtihani huu muhimu. Hii ni ndoto iliyoleta matumaini makubwa kwa shule, wazazi, walimu na serikali kwa ujumla, kwa kuonyesha kuwa juhudi za kuboresha ubora wa elimu zinaendelea kuleta matunda chanya.
Mtihani wa Kumaliza Elimu ya Msingi ni hatua muhimu katika mfumo wa elimu nchini Tanzania. Ni mtihani unaochagiza vipaji na kukuza maarifa ya msingi kwa watoto wa shule za msingi. Kupitia mtihani huu, wanafunzi huthibitisha uelewa wao wa masomo mbalimbali yenye lengo la kuwajengea msingi imara wa kujiendeleza kwenye ngazi za elimu za sekondari na zaidi.
Kuangalia matokeo hayo tafadhali bofya linki zifuatazo hapo chini:
- Matokeo ya Darasa la Saba 2025/2026
- NECTA PSLE Results
- PSLE-2025 EXAMINATION RESULTS
- Primary School Examination Results (psle) 2025
| ARUSHA | DAR ES SALAAM | DODOMA |
| IRINGA | KAGERA | KIGOMA |
| KILIMANJARO | LINDI | MARA |
| MBEYA | MOROGORO | MTWARA |
| MWANZA | PWANI | RUKWA |
| RUVUMA | SHINYANGA | SINGIDA |
| TABORA | TANGA | MANYARA |
| GEITA | KATAVI | NJOMBE |
| SIMIYU | SONGWE |

