Kila mwaka, wanafunzi wa kidato cha nne nchini Tanzania husubiri kwa hamu matokeo ya uchaguzi wa kujiunga na kidato cha tano, maarufu kama Form Five Selection. Mchakato huu unaendeshwa na Ofisi ya Rais – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) kwa kushirikiana na Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA). Uchaguzi huu ni hatua muhimu inayowawezesha wanafunzi kuendelea na elimu ya sekondari ya juu au kujiunga na vyuo vya kati, kulingana na matokeo yao ya mtihani wa taifa wa kidato cha nne (CSEE).
Mchakato wa Form Five Selection 2025
Sifa na Vigezo Vinavyotumika Kufanya Uchaguzi wa Wanafunzi Kujiunga Kidato cha Tano na Vyuo Vya Kati
Katika mchakato wa uchaguzi wa wanafunzi kujiunga na kidato cha tano na vyuo vya kati kwa mwaka 2025, TAMISEMI hutumia vigezo mbalimbali kuhakikisha uwazi na haki kwa wote. Vigezo hivi ni pamoja na:
- Ufaulu wa Masomo: Mwanafunzi anatakiwa kuwa na angalau alama za A, B, au C katika masomo yasiyo ya dini, ikiwa ni kiashiria cha uwezo wake kitaaluma.
- Tahasusi Aliyochagua: Uchaguzi wa masomo maalum (tahasusi) ni kipengele muhimu, kwani huathiri shule atakayopangiwa mwanafunzi.
- Upatikanaji wa Nafasi: Idadi ya nafasi katika kila shule huathiri mchakato wa upangaji, hasa katika shule zenye ushindani mkubwa.
- Umri wa Mwanafunzi: Mwanafunzi anatakiwa kuwa na umri wa chini ya miaka 25 ili kupangiwa nafasi ya kidato cha tano katika shule za serikali.
Tarehe ya Kutangazwa kwa Majina ya Selection za Form Five
Kwa kawaida, TAMISEMI hutangaza majina ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha tano miezi michache baada ya matokeo ya kidato cha nne kutangazwa na NECTA. Kwa kuzingatia utaratibu wa miaka ya nyuma Majina ya form five selection yalitangazwa kama ifuatavyo:
- 2019: Matokeo yalitangazwa Tarehe 01 June 2019.
- 2020: Matokeo yalitangazwa Tarehe 17 June 2020.
- 2021: Matokeo yalitangazwa Juni 1, 2021
- 2022: Matokeo yalitangazwa May 12, 2022.
- 2023: Matokeo yalitangazwa Juni 11, 2023.
- 2024: Matokeo yalitangazwa Trehe 30 Mei 2024.
Kwa mwaka 2025, inatarajiwa kwamba majina ya waliochaguliwa yatatangazwa kati ya Mei 31 hadi Juni 15, 2025.
Jinsi ya Kuangalia Waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Tano [Form five selection]
Kama mzazi au mwanafunzi, unaweza kufuatilia majina ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha tano na vyuo mwaka 2025 kwa kupitia linki maalum za mikoa. Zifuatazo ni hatua za kufuata:
Hatua ya 1: Kutembelea Tovuti Rasmi ya TAMISEMI ya Uchaguzi wa Wanafunzi wa Kidato cha Tano na Vyuo Vya Kati
- Tembelea tovuti rasmi ya TAMISEMI: Nenda kwenye https://selform.tamisemi.go.tz/content/selection-and-allocation/.
- Bofya linki ya “Form Five First Selection, 2025”: Baada ya kufungua tovuti, tafuta na ubofye sehemu inayosema “Form Five First Selection, 2025”.
Hatua ya 2: Chagua Linki ya Mkoa Ulikosoma
- Orodha ya mikoa: Baada ya kufungua linki ya “Form Five First Selection, 2025”, utakutana na orodha ya mikoa yote Tanzania.
- Chagua mkoa: Bonyeza jina la mkoa ambapo mwanafunzi alifanya mtihani wa kidato cha nne.
Hatua ya 3: Chagua Linki ya Halmashauri Ulikosoma
- Orodha ya halmashauri: Baada ya kuchagua mkoa, orodha ya halmashauri zote katika mkoa husika itajitokeza.
- Chagua halmashauri: Bonyeza jina la halmashauri ambapo shule ya mwanafunzi ipo.
Hatua ya 4: Chagua Shule Uliyosoma
- Orodha ya shule: Baada ya kuchagua halmashauri, orodha ya shule zote katika halmashauri hiyo itajitokeza.
- Chagua shule: Bonyeza jina la shule ambayo mwanafunzi alifanya mtihani wa kidato cha nne.
Hatua ya 5: Angalia Orodha ya Majina na Pakua Maelekezo ya Kujiunga (Joining Instructions PDF)
- Orodha ya majina: Baada ya kuchagua shule, orodha ya majina ya wanafunzi waliochaguliwa pamoja na shule walizopangiwa itajitokeza.
- Pakua maelekezo ya kujiunga: Unaweza kupakua “Joining Instructions” ya shule husika (kama PDF) kupitia linki ya jina la shule mbele ya namba na jina la mwanafunzi.
Hatua ya 6: Kuhakikisha Taarifa
- Thibitisha taarifa: Hakikisha unachunguza majina kwa umakini ili kuthibitisha kama mwanafunzi amechaguliwa na wapi.
Ikiwa kuna matatizo yoyote au maswali zaidi, unashauriwa kuwasiliana na ofisi za elimu za mkoa husika au kutumia namba za msaada zilizotolewa katika tovuti husika.
Majina ya Wanafunzi Waliochaguliwa Kujiunga na form five na Vyuo 2025 kwa Kila Mkoa
Hapa chini ni orodha ya linki za mikoa kwa ajili ya kuangalia majina ya waliochaguliwa kujiunga na kidato cha tano:
Mkoa |
Arusha |
Dar es Salaam |
Dodoma |
Geita |
Iringa |
Kagera |
Katavi |
Kigoma |
Kilimanjaro |
Lindi |
Manyara |
Mara |
Mbeya |
Morogoro |
Mtwara |
Mwanza |
Njombe |
Pwani |
Rukwa |
Ruvuma |
Shinyanga |
Simiyu |
Singida |
Songwe |
Tabora |
Tanga |
Hitimisho
Uchaguzi wa wanafunzi kujiunga na kidato cha tano kwa mwaka 2025 ni hatua muhimu katika safari ya elimu ya mwanafunzi. Ni muhimu kufuatilia kwa karibu matangazo rasmi kutoka TAMISEMI na kufuata hatua zilizoainishwa ili kuhakikisha unapata taarifa sahihi na kwa wakati. Kwa msaada zaidi, wasiliana na ofisi za elimu za mkoa husika au tembelea tovuti rasmi ya TAMISEMI.