Katika mfumo wa elimu nchini Tanzania, Mtihani wa darasa la saba ndio msingi kwa wanafunzi wanaotarajia kuendelea na elimu ya sekondari. Kila mwaka, maelfu ya wanafunzi kutoka mikoa mbalimbali nchini hushiriki katika mtihani huu wa kitaifa, ambao matokeo yake hutumika na Baraza la Mitihani la Tanzania katika upangaji wa shule na uchaguzi wa wanafunzi kujiunga na kidato cha kwanza kwa mwaka unaofuata. Matokeo ya darasa la saba kwa mwaka 2024/2025 yanasubiriwa kwa hamu kubwa sana na wanafunzi, wazazi, walimu, Pamoja na wadau mbalimbali.
SOMA NA HII: Haya hapa Matokeo ya Darasa la Saba 2024 Zanzibar (ZEC Standard Seven 2024 results)
Kwa kawaida, matokeo haya hutangazwa na Baraza la Mitihani la Tanzania (NECTA), ambalo ndio linalosimamia maandalizi, usimamizi, na utangazaji wa mitihani ya taifa. Katika makala hii, tutazungumzia kwa kina hatua za jinsi ya kuangalia matokeo ya darasa la saba kwa mwaka wa masomo 2024/2025, Muda na Tarehe rasmi za Kutangazwa kwa Matokeo, Tafsiri ya Alama na Madaraja ya Matokeo ya Darasa la saba na Uchaguzi wa Kidato cha kwanza 2025
Muda na Tarehe za Kutangazwa kwa Matokeo darasa la saba 2024
NECTA hutangaza matokeo ya mitihani ya darasa la saba kila mwaka kati ya Mwishoni mwa mwezi Novemba na Desemba. Hata hivyo, tarehe halisi ya kutangazwa kwa matokeo ya mwaka 2024/2025 itatangazwa rasmi kupitia tovuti NECTA.
Table of Contents
Kutangazwa kwa matokeo ya darasa la saba ni tukio muhimu linalofuatiliwa na wadau wengi kwa hamu kubwa hapa nchini. Kwa kawaida, tarehe maalum ya kutangazwa matokeo haya, hutegemeana na ratiba ya kitaifa ya mitihani na ukamilishaji wa mchakato wa uchambuzi na upangaji wa matokeo ya mitihani.
Wakati NECTA ikijiandaa kutoa tangazo rasmi kuhusu tarehe husika, ni muhimu kwa wanafunzi, wazazi, na walimu kufuatilia habari kupitia vyombo vya habari kama vile redio, televisheni, pamoja na tovuti rasmi ya NECTA ili kupata taarifa za kuaminika kuhusu tarehe na muda rasmi wa kutangazwa kwa matokeo hayo.
01
of 02
Jinsi ya Kuangalia Matokeo ya Darasa la Saba 2024/2025 Kupitia Tovuti ya NECTA
Katika zama hizi za kidijitali, mchakato wa kutazama matokeo ya mtihani kupitia mtandao ni umekuwa rahisi sana ambapo wanafunzi na wadau wa elimu wanaweza kupata taarifa ya matokeo kwa haraka na kwa urahisi.
Ikiwa unatamani kufahamu matokeo ya darasa la saba kwa mwaka 2024, Tovuti ya Baraza la Mitihani la Tanzania (NECTA) ndio jukwaa rasmi na lenye kuaminika kwaajili ya kutazama matokeo ya darasa la saba. Ufuatao ni mwongozo kamili wa hatua kwa hatua wa jinsi ya kuangalia matokeo ya darasa la saba kupitia tovuti ya NECTA
Hatua ya 1: Kutembelea Tovuti Rasmi ya NECTA
- Fungua kivinjari cha intaneti katika simu yako au kompyuta
- Andika moja kwa moja anwani ya tovuti ya NECTA, ambayo ni www.necta.go.tz.

Hatua ya 2: Chagua Kipengele cha Matokeo:
- Mara tu baada ya kuingia kwenye tovuti ya NECTA, Nenda kwenye Menyu kuu na tafuta sehemu iliyoandikwa “Matokeo” au “Results.”
- Bonyeza kwenye kipengele cha “Results”.
- Menyu ndogo ya kushuka chini itajitokeza, Bonyeza kwenye kiungo kilichoandikwa PSLE kitakachokupeleka kwenye ukurasa rasmi wa matokeo darasa la saba (PSLE Results).

Hatua ya 3: Chagua Mtihani wa Darasa la saba kwa Mwaka 2024
- Ukurasa wa matokeo ya darasa la saba utakupa orodha ya mitihani kwa miaka mbalimbali.
- Bonyeza au chagua linki ya mtihani wa mwaka 2024

Hatua ya 4: Tazama matokeo kwa mikoa yote
- Baada ya kuchagua na kubonyeza linki ya mwaka husika,
- Utapelekwa kwenye ukurasa rasmi wa matokeo yote ya darasa la saba kwa mwaka 2024
- Hapa utaweza kupata matokeo ya darasa la saba kwa ngazi ya miko yote
- Tafuta na bonyeza kwenye kiunganisho cha Jina la mkoa husika ili kuatazama matokeo katika mkoa husika

Hatua ya 5: Angalia Matokeo yako
- Mara baada ya kubonyeza linki ya mkoa husika,
- Ukurasa mwingine wa matokeo katika mpangilio wa wilaya katika mkoa huo utafunguka
- Bonyeza linki au kiunganishi cha matokeo ya wilaya husika ili kuangalia matokeo katika wilaya hiyo
- Baada ya kubonyeza linki au kiunganishi cha wilaya husika, utaona orodha ya shule zote katika wilaya hiyo
- Tafuta shule uliyofanyia mtihani wako, na bonyesha kwenye linki ya shule hiyo
- Baada ya kufanya hivyo, ukurasa mwingine wenye matokeo ya shule hiyo utafunguka, kuangalia matokeo yako tafuta jina mwanafunzi
- Matokeo ya mtahiniwa yatatokea kwenye skrini, yakionyesha alama zake katika masomo mbalimbali.

Hatua ya 6: Pakua na Chapisha matokeo yako
Ikiwa unahitaji kuwa na nakala ya matokeo yako kwa ajili ya matumizi ya baadaye, unaweza kupakua matokeo hayo au kuchapisha matokeo moja kwa moja kutoka katika tovuti kwa kubonyeza kitufe cha “Print” au “Save as pdf.”

Kwa kufuata hatua hizi rahisi, wanafunzi na wazazi wanaweza kupata matokeo kwa haraka na kwa wakati.
02
of 02
Matokeo darasa la saba kimkoa (mikoa yote)
NECTA hutoa matokeo ya darasa la saba kwa mpangilio wa kila mkoa. Matokeo ya mikoa yote yanapatikana kwenye tovuti ya NECTA, pia, unaweza kuyatazama kupitia viunganishi au linki za mikoa hapo chini:
ARUSHA | DAR ES SALAAM | DODOMA |
IRINGA | KAGERA | KIGOMA |
KILIMANJARO | LINDI | MARA |
MBEYA | MOROGORO | MTWARA |
MWANZA | PWANI | RUKWA |
RUVUMA | SHINYANGA | SINGIDA |
TABORA | TANGA | MANYARA |
GEITA | KATAVI | NJOMBE |
SIMIYU | SONGWE |
Tafsiri ya Alama na Madaraja Katika Matokeo ya Darasa la saba 2024
NECTA hutoa alama kulingana na ufaulu wa mwanafunzi katika mitihani yake, ambapo kila alama inawakilisha kiwango cha ufahamu ulioonyeshwa. Madaraja yanatoa mwonekano wa jumla ya utendaji na yanaweza kuwa kiashiria cha shule anazostahili mwanafunzi.
Baada ya kutazama matokeo ya darasa la saba kwa umakini, ni muhimu kuelewa maana ya alama na madaraja mbalimbali yaliyotumika katika matokeo hayo. Hii itakusaidia wewe wanafunzi, mazazi, na mwalimu kuamua hatua inayofuata ya kielimu na kuelewa maendeleo ya mwanafunzi. Ufuatao ni mwongozo wa alama na madaraja yanayotumika katika matokeo ya darasa la saba:
GREDI | ALAMA | MAELEZO |
A | 75-100 | Bora sana (Excellent): Hii ina maanisha kiwango bora zaidi ambacho mwanafunzi ameonyesha uelewa wa hali ya juu na uwezo wa kutumia maarifa kwa usahihi. |
B | 65-74 | Vizuri sana (Very Good): Hii inamaanisha uelewa mzuri ambapo mwanafunzi ameonyesha uwezo wa kutosha katika somo husika. |
C | 45-64 | Vizuri (Good): Kiwango hiki kinaonyesha uhusiano wa wastani wa uelewa na utekelezaji katika somo. Ni kiwango kinachokubalika lakini kuna nafasi ya kuboresha |
D | 30-44 | Inaridhisha (Satisfactory): Mwanafunzi ameonyesha kiwango cha kawaida cha uelewa katika somo husika. Mwanafunzi amefanikiwa kufikia kiwango cha chini kinavyohitajika katika ufaulu, lakini bado hajaonyesha umahiri au uelewa wa kina. |
F | 0-29 | Feli (Fail): Hii inaonyesha kuwa mwanafunzi amepata alama ya chini ya kiwango kinachohitajika na huenda akahitajika kurudia mtihani au kushiriki masomo ya ziada |
Muongozo na utaratibu wa Kujiunga na Shule za Sekondari Baada ya Matokeo (Uchaguzi wa Kidato cha kwanza 2025)
Baada ya matokeo ya mtihani wa darasa la saba kutangazwa, wazazi na wanafunzi wanasubiri kwa hamu kujua shule za sekondari ambazo Watoto wao watapangiwa. Baada ya matokeo kutangazwa, TAMISEMI kwa kushirikiana na NECTA hufanya zoezi la kuwapanga wanafunzi katika shule mbalimbali za sekondari za seriakali kulingana na madaraja waliyopata katika matokeo yao.
Mchakato wa upangaji wa wanafunzi katika kidato cha kwanza kwa mwaka 2025 unatarajiwa kukamilika kufikia mwezi Disemba, hivyo wazazi na wanafunzi wategemee kuwa TAMISEMI na NECTA watatangaza majina ya wanafunzi waliopangiwa kidato cha kwanza mapema mwezi Disemba ili wazazi waweze kukamilisha maandalizi ya mahitaji ya wanafunzi waliochaguliwa kwa wakati.
Maswali Yanayoulizwa Mara kwa Mara Kuhusu Matokeo ya Darasa la Saba
Matokeo ya mtihani wa darasa la saba husubiriwa kwa hamu na wanafunzi, wazazi, na walimu hapa nchini. Yafuatayo ni baadhi ya maswali yanayoulizwa mara kwa mara pamoja na majibu yake kuhusu matokeo haya:
1. Je, matokeo ya darasa la saba 2024 yanatoka lini?
Matokeo haya kwa kawaida hutangazwa katika kipindi cha robo ya mwisho ya mwaka, mara nyingi kuanzia mwezi wa Oktoba hadi Novemba. Hata hivyo, tarehe rasmi itatolewa na NECTA, unashauriwa kufuatilia kwa ukaribu tovuti ya NECTA kwa taarifa rasmi na habari zenye uhakika kuhusu matokeo hayo.
2. Inachukua muda gani baada ya mtihani hadi matokeo kutangazwa?
Kwa kawaida, matokeo hutangazwa takriban miezi miwili (2) hadi mitatu (3) baada ya mitihani kufanyika. Katika Kipindi hiki NECTA hujipatia muda wa kutosha kukusanya, kusahiisha, na kuchakata matokeo kabla ya kuyatangaza rasmi.
2. Je, matokeo yanaweza kubadilika baada ya kutangazwa?
Mara nyingi matokeo yanayotangazwa huwa ni ya mwisho, hata hivyo kuna uwezekano wa mabadiliko kufanyika ikiwa kuna makosa yalitokea wakati kusahisha au uchakataji wa matokeo ya mitihani. NECTA inaweza kukagua upya matokeo yako iwapo kutakuwa na maombi maalum na lenye sababu za msingi na zenye mashiko.
3. Je, kuna ada yoyote katika kuangalia matokeo darasa la saba 2024 mtandaoni au kupitia simu?
Hakuna gharama au ada yoyote inayohitajika Ili kutazama matokeo yako kupitia tovuti rasmi ya NECTA. Hata hivyo, matumizi ya huduma za USSD kupitia simu za mkononi yanaweza kuhusisha gharama za mawasiliano (Gharama kwa kila SMS ni Tshs 100/= kwa huduma za USSD)