Table of Contents
Katika dunia ya sasa, teknolojia imekuwa na mchango mkubwa katika kuboresha huduma za mbalimbali kwa jamii, na Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) nchini Tanzania inachukua hatua muhimu katika kuimarisha mchakato wa usajili wa vitambulisho vya taifa. Mfumo wa maombi ya NIDA mtandaoni unawawezesha raia wa Tanzania na wageni wa makazi kujaza fomu za maombi kwa urahisi na kwa haraka, bila kuwa na changamoto ya kutembea umbali mrefu hadi ofisi za NIDA.
Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) ilianzishwa nchini Tanzania kwa lengo la kuimarisha usajili na utoaji wa vitambulisho vya kitaifa kwa raia na wakazi wa nchi hii. Kuanzia mwaka wa 2014, NIDA imekuwa ikitoa mfumo wa kisasa wa usajili wa vitambulisho vya taifa, ambapo mwombaji ana uwezo wa kujaza fomu za maombi kwa njia ya kielektroniki (online). Mfumo huu umerahisisha utaratibu wa usajili, na kufanya rahisi kwa mtu yeyote kujaza na kutuma maombi ya Kitambulisho cha NIDA Online bila kufanya safari ndefu hadi ofisi za NIDA.
Usajili kwa njia ya mtandao unavutia watu wengi kutokana na urahisi na ufanisi wake. Kila mwananchi au mgeni mkazi anaweza kujaza fomu ya maombi ya kitambulisho cha taifa akiwa nyumbani au mahali popote alipo. Hii ni huduma muhimu ambayo inachangia katika uhakika wa utambulisho wa raia na wakazi, ikiwa ni pamoja na kuimarisha usalama wa taifa.
Ili kupata kitambulisho cha NIDA, mwombaji anapaswa kufuata hatua mbalimbali, kuanzia kujaza taarifa mbalimbali katika mfumo wa mtandaoni, kuchapisha fomu iliyokamilika, na kuwasilisha pamoja na vielelezo vya utambulisho katika ofisi za NIDA zilizopo karibu. Mfumo huu wa maombi ya kitambulisho cha taifa umekuwa na mafanikio makubwa, sawa na malengo yaliyokusudiwa, na umetengeneza mazingira mazuri ya ushirikiano kati ya serikali na raia. Uwezekano wa kujiandikisha mtandaoni unarahisisha mchakato wa upatikanaji wa kitambulisho, na hivyo kuleta matumizi mazuri ya teknolojia katika utawala wa umma nchini Tanzania.

1 Mahitaji Muhimu Kabla ya Kujiandikisha au Kufanya usajili mtandaoni
Kabla ya kuanza mchakato wa kujiandikisha mtandaoni kupitia Mfumo wa NIDA, ni muhimu kuhakikisha unaviandaa na kuvichunguza vyema vielelezo vyote vinavyohitajika. Hapa kuna orodha ya mahitaji muhimu ambayo kila mwombaji anapaswa kuwa navyo kabla ya kuanza mchakato wa usajili:
- Cheti cha kuzaliwa cha mwombaji
- Nakala ya cheti cha kuzaliwa / kiapo cha mzazi mmoja.
- Kama uraia wa mwombaji ni wakurithi: thibitisha kwa nakala ya cheti cha kuzaliwa au nakala ya kitambulisho cha Taifa cha mzazi mmoja.
- Kama uraia wa mwombaji ni wa kujiandikisha, thibitisha kwa nakala ya uraia wa kujiandikisha (Dossier Number) ya mwombaji.
Kwa kuhakikisha unakuwa na nyaraka hizi kabla ya kuanza mchakato wa kujiandikisha, utaweza kufanya mchakato huu kwa urahisi na kwa ufanisi zaidi. Hii itasaidia kuepusha ucheleweshaji wowote katika kupata kitambulisho chako cha taifa kutoka NIDA.
2 Mambo Muhimu ya Kuingia Wakati wa Ujazaji Fomu
Wakati wa mchakato wa kujiandikisha mtandaoni kupitia Mfumo wa NIDA, kuna mambo kadhaa muhimu ambayo kila mwombaji anapaswa kuzingatia ili kuhakikisha usajili unakamilika kwa urahisi na ufanisi. Hapa chini ni masuala ya msingi ambayo yanapaswa kufuatiliwa:
- Mwombaji anatakiwa kuwa na anuani ya barua pepe ambayo ataitumia kujisajili na kupokea kiunga kitakachomuwezesha kukamilisha usajili wake.
- Mwombaji anatakiwa kuwa na nyaraka zisizopungua mbili zitakazotumika kuthibitisha utambulisho wake. Mfano wa nyaraka hizo ni; Cheti cha kuzaliwa n.k.
- Mwombaji anatakiwa kufanya “scanning” ya nyaraka zake na kuziweka katika muundo wa PDF (usiozidi kurasa moja kwa kila kiambatisho) au picha katika muundo wa JPG au PNG.
- Ni muhimu Mwombaji kujaza Namba yake ya simu ya mkononi.
- Mwombaji anatakiwa kuambatisha cheti cha kuzaliwa endapo amezaliwa Mwaka 1980 na kuendelea. Aidha, endapo Mwombaji amezaliwa kabla ya mwaka 1980 anatakiwa kuambatisha cheti cha kuzaliwa au “Affidavit”.
- Kwa Waombaji wenye majina mengine; ni vyema kuandika majina hayo ili endapo ikatokea uhitaji wa kurekebisha majina yake iwe rahisi kutambulika.
- Mwombaji anatakiwa kufahamu majina ya Baba na Mama yake mzazi.
- Mwombaji ambaye ana Namba za Utambulisho (NIN) za wazazi wake; anatakiwa kuweka viambata halisi (kwa wazazi waliokwishapata vitambulisho vya Taifa).
- Mwombaji anatakiwa kujua namba ya Nyumba, Mtaa na kata anayoishi.
- Kwa Watanzania walioko nje ya Nchi, wanatakiwa kupata uthibitisho wa ukaazi katika Nchi husika kutoka kwa Afisa wa Ubalozi wa Tanzania ili kujaza sehemu ya makazi, Mtaa/Kata kwa usahihi.
- Endapo Mwombaji amepata vyeti vya Shule, Namba ya mlipa kodi (TIN) na Kadi ya mpiga kura; ni vyema kuambatanisha.
- Mwombaji anatakiwa kujaza Fomu kwa usahihi na kuhakikisha viambata vyake na taarifa alizo jaza katika mfumo hazikinzani na taarifa nyingine, kama vile taarifa za Shule au Biashara.
- Mwombaji anatakiwa kujaza taarifa zake kwa usahihi, na kuchapisha taarifa hizo katika fomu na kwenda kwenye Ofisi ya Serikali ya Mtaa napoishi kwa ajili ya kugongewa Mhuri na Saini ya Mwenyekiti wa Mtaa wake.
- Mwombaji anatakiwa kufika katika Ofisi ya NIDA iliyoko kwenye Wilaya yake ya makazi akiwa na fomu iliyokamilika (Fomu iliyogongwa Mhuri na kuwekwa Saini ya Mwenyekiti wa Serikali wa Mtaa), pamoja na nakala ngumu za viambatisho vyake alivyopakia katika mfumo wakati wa usajili kwa ajili ya kukamilisha taratibu za usajili.
- Kwa Mwombaji ambaye anahitaji kupata maelezo ya ziada; asisite kufika katika ofisi ya NIDA iliyopo karibu.
Kwa kuzingatia mambo haya muhimu, utakuwa na nafasi kubwa ya kufanikiwa katika mchakato wa kujisajili mtandaoni na kupata kitambulisho chako cha nchi kupitia NIDA bila matatizo yoyote. Hii itakusaidia kujiimarisha zaidi katika jamii na kupata huduma mbalimbali zinazohitaji kitambulisho cha taifa.
3 Hatua za Kujisajili Mtandaoni
Kujisajili mtandaoni kupitia Mfumo wa NIDA ni mchakato rahisi unaofuata hatua kadhaa ambazo kila mwombaji anapaswa kuzifuata ili kuhakikisha wanafanikiwa katika kupata kitambulisho cha taifa. Hapa kuna hatua za kina za kujisajili:

1. Tembelea Tovuti ya Mfumo wa maombi ya Kitambulisho cha Taifa NIDA (https://eonline.nida.go.tz/)
Hatua ya kwanza ni kutafuta tovuti rasmi ya NIDA. Hakikisha unatumia tovuti iliyo sahihi ili kuepuka tovuti za udanganyifu.
2. Fungua Akaunti
Mara baada ya kufika kwenye tovuti, bofya kwenye kitufe cha “Jisajili au Create Account” au tumia linki https://eonline.nida.go.tz/Account/Register ili kupata fomu ya usajili. Jaza maelezo muhimu yaliyoombwa, ikiwa ni pamoja na barua pepe na nenosiri. Na hakikisha nenosiri linakidhi vigezo vilivyowekwa.
3. Thibitisha Barua Pepe
Baada ya kujaza fomu ya usajili, utapokea barua pepe ya uthibitisho. Fungua barua pepe hiyo na fuata kiungo kilichomo ili kukamilisha mchakato wa ufunguzi wa akaunti yako.
4. Jaza Fomu ya Maombi
Baada ya kuthibitisha akaunti yako, ingia kwenye mfumo kwa kutumia akaunti yako. Kisha, jaza fomu ya maombi ya kitambulisho cha taifa. Hakikisha unajaza maelezo yote kwa usahihi na ni muhimu kuzingatia viambatanisho vyako.
5. Tuma Maombi
Mara baada ya kumaliza kujaza fomu na kuangalia kwa makini taarifa zako, tuma maombi yako. Utapokea ujumbe wa kuthibitisha kuwa maombi yako yamepokelewa.
6. Tembelea Ofisi ya NIDA
Baada ya kutuma maombi, chukua fomu iliyochapishwa pamoja na vielelezo vyako vya uthibitisho na tembelea ofisi ya NIDA iliyoko katika eneo lako. Hakikisha unaelewa na kufuata taratibu zinazohitajika ili kukamilisha usajili wa alama za biometria.
7. Ufuatiliaji wa Maombi
Baada ya kukamilisha hatua za usajili, unaweza kufuatilia maendeleo ya maombi yako kupitia mfumo wa mtandaoni. Mfumo huu utakuwezesha kujua hali ya maombi yako na muda unaokadiriwa kukamilika.
Kwa kufuata hatua hizi kwa umakini, unaweza kufanikiwa kwenye mchakato wa kujisajili mtandaoni na kupata kitambulisho chako cha NIDA bila usumbufu mkubwa.
4 Fomu ya maombi ya kitambulisho cha NIDA kwa maombi ya kawaida
Ikiwa unapendelea utaratibu wa kawaida wa maombi ya kitambulisho cha utaifa utatakiwa kupakua na kujaza fomu ya maombi ya Utambulisho wa Taifa Namba 1A: Jaza fomu ya maombi ya Utambulisho wa Taifa Namba 1A kwa kalamu ya wino mweusi na kwa herufi kubwa. (Fomu inapatikana kwenye ofisi ya Usajili ya NIDA, Wilayani/Serikali ya Mtaa na kwenye tovuti ya NIDA)
DOWNLOAD : fomu ya maombi ya Utambulisho wa Taifa Namba 1A
Hakikisha una saini fomu yako ya maombi ya Utambulisho wa Taifa kwenye kipengele Namba 59/60 ama umeweka alama ya dole gumba iwapo hauna saini rasmi ama hujui kusoma na kuandika,
Gonga muhuri fomu yako ya Maombi ya Utambulisho wa Taifa kwenye Serikali ya Mtaa unakoishi kipengele namba 59/60 na kuandikiwa barua ya utambulisho wa makazi,
Ambatisha nyaraka zifuatazo, viambatisho hivi ni vya lazima:
i. Cheti cha kuzaliwa,
ii. Barua ya utambulisho wa makazi kutoka Serikali ya Mtaa unakoishi,
iii. Cheti cha kuzaliwa au Kitambulisho cha Taifa cha mzazi mmoja.
Ambatisha viambatisho vya ziada ulivyonavyo kati ya vifuatavyo:
i. Vyeti vya Masomo-Msingi,Sekondari,Chuo,
ii. Pasi ya kusafiria,
iii. Leseni ya udereva,
iv. Namba ya utambulisho wa mlipa kodi (TIN),
v. Kadi ya bima ya afya,
vi. Kitambulisho cha mzanzibar mkaazi
Wasilisha fomu yako ya maombi kwenye Ofisi ya Usajili ya NIDA wilaya unakoishi kwa ajili ya kuchukuliwa alama za kibaiolojia (kupigwa picha, kuweka saini ya kielektroniki na kuchukuliwa alama za vidole) ili kupisha hatua zinazofuata ziendelee.
Mavazi ya kuzingatia wakati wa Usajili: Ili picha ya mwombaji wa Utambulisho wa Taifa itoke katika ubora uliokusudiwa pindi unapowasilisha fomu ya maombi kwenye ubalozi husika kupigwa picha na kuchukuliwa alama za vidole, unashauriwa kutovaa nguo; nyeupe, kijivu, bluu mpauko, pinki au nguo za kung’aa, jezi, nguo zenye nembo, michoro au maandishi, kofia aina yoyote na kutopaka hina viganjani ili alama za vidole zisomeke kirahisi,
Hatua mbalimbali za usajili na utambuzi wa watu:-
i. Ujazaji wa fomu za Utambuzi na Usajili,
ii. Uhakiki wa awali wa fomu za maombi,
iii. Uingizaji wa taarifa kwenye mfumo wa kompyuta,
iv. Kuthibitishaji taarifa za mwombaji zilizo katika mfumo wa kompyuta,
v. Uchukuaji wa alama za vidole, picha na saini ya kielektroniki,
vi. Utengenezaji wa Daftari Kuu la Taarifa za Watu,
vii. Uhakiki wa mwisho,
viii.Uchapishaji, uhakiki wa ubora na Utoaji wa Vitambulisho vya Taifa.
Ufafanuzi wa mambo msingi hitajika kwa baadhi ya hatua za usajili tajwa hapo juu;
Usajili – Ujazaji wa fomu (biographic data)
Mwombaji wa Kitambulisho Raia, Mgeni ama Mkimbizi anatakiwa kufika katika kituo/ofisi ya usajili na vivuli (Copy) ya nyaraka za kutambulisha makazi, uraia na umri wake kama ilivyoainishwa hapo juu katika kipengele cha mahitaji ya kila kundi wakati wa usajili.
Uchukuaji alama za kibaiolojia
Hatua hii ya Usajili inajumuisha upitiaji wa taarifa za mwombaji katika mfumo, uchukuliwaji wa alama za vidole, picha na utiaji wa saini ya kielektroniki ambapo kuna mambo msingi ya mwombaji kuzingatia ambayo ni;
Kwa ajili ya ubora na mwonekano mzuri wa picha mwombaji unashauriwa kutovaa nguo nyeupe, pinki, kijivu, bluu mpauko au nguo zenye rangi za kungaa sana. Kutovaa kofia ya aina yoyote wakati wa kupiga picha, au kupaka hina viganjani wakati wa uchukuaji wa alama za kibaiolojia.
Ili kurahisisha zoezi hili, mwombaji unaombwa kufika kwenye ofisi/kituo cha usajili na nyaraka halisi (original) za kuthibitisha uraia na umri wake mathalani, cheti cha kuzaliwa, pasipoti, vyeti vya elimu ya msingi na sekondari, leseni ya udereva, kitambulisho cha bima ya afya, kitambulisho cha mpigakura na kitambulisho cha mzanzibar mkazi.
Ugawaji Vitambulisho vya Taifa
Mwombaji anatakiwa kufika katika ofisi ya usajili katika wilaya husika ama kulingana na maelekezo/matangazo yanayotolewa katika eneo hilo ili kupatiwa kitambulisho chake kwa kuzingatia kuja na risiti maalumu aliyopatiwa na NIDA wakati alipokamilisha kuchukuliwa alama za kibaiolojia.
5 Msaada na Huduma kwa Wateja
Wakati wa mchakato wa kujisajili mtandaoni kupitia Mfumo wa NIDA, ni muhimu kujua jinsi ya kupata msaada na huduma kwa wateja, Kwa maelezo zaidi, tafadhali fika kwenye Ofisi ya Usajili ya NIDA Wilayani au wasiliana na NIDA kupitia Namba: 0752 000 058, 0687 088 888, 0777 740 006, 0677 146 666. Tovuti www.nida.go.tz, Barua pepe info@nida.go.tz, Facebook, Instagram, Twitter Nidatanzania