Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi anapenda kuwatangazia Watanzania wote wenye sifa kuomba Ajira ya Mwandishi Mwendesha Ofisi Daraja la II. Tangazo hili ni baada ya kupokea kibali cha Ajira Mbadala chenye Kumb. Na. FA.228/613/01F/028 cha tarehe 21 Januari, 2025 toka kwa Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala bora.
Mchanganuo wa nafasi ni kama ifuatavyo:
MWANDISHI MWENDESHA OFISI II – NAFASI MOJA (1)
KAZI NA MAJUKUMU
- Kuchapa barua, taarifa na nyaraka za kawaida na siri
- Kupokea wageni na kuwasikiliza shida zao na kuwaelekeza sehemu wanapoweza kushughulikiwa
- Kutunza taarifa/kumbukumbu za matukio, miadi, tarehe za vikao, safari za Mkuu wake na ratiba ya kazi zingine
- Kutafuta majalada na nyaraka zinazohitajika katika utekelezaji wa majukumu ya kazi
- Kupokea majalada na kusambaza kwa maofisa walio katika Idara/ Kitengo/ Sehemu husika
- Kukusanya, kutunza na kuyarejesha majalada na nyaraka sehemu zinazohusika
- Kupanga dondoo na kufanya maandalizi ya Vikao mbalimbali
- Kuandaa orodha ya mahitaji ya vifaa vya Ofisi
- Kufanya kazi zingine atakazopangiwa na Mkuu wake wa kazi
SIFA ZA MWOMBAJI
- Awe na Elimu ya Kidato cha nne au sita mwenye Stashahada ya Uhazili au Cheti cha NTA level 6 ya Uhazili.
- Aidha awe amefaulu somo la Hatimkato ya Kiswahili na Kingereza maneno 100 kwa dakika moja nakupata program za Komputa za Ofisi kama Word, Excel, PowerPoint, E-mail na Publisher kutoka Chuo chochote kinachotambulika na Serikali.
Mshahara
Mshahara atalipwa kwa kuzingatia viwango vya Serikali TGS C
MASHARTI YA JUMLA KWA WAOMBAJI
- Waombaji wote wawe ni Raia wa Tanzania na wenye Umri kati ya miaka 18 hadi 45 isipokuwa kwa wale tu walioko kazini Serikalini.
- Waombaji wenye ulemavu wanahamasishwa kutuma maombi na wanapaswa kuainisha kwenye Mfumo wa kuombea ajira ulemavu walionao kwa ajili ya taarifa kwa Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma.
- Waombaji wote waambatanishe maelezo binafsi yaliyojitosheleza (Detail Curriculum Vitae) yenye anuani inayotumika, namba za simu zinazopatikana na anuani ya barua pepe (E-mail Address) pamoja na majina ya wadhamini (Referees) watatu wa kuaminika.
- Maombi yote yaambatane na vyeti vya Elimu na Taaluma vilivyothibitishwa na Mwanasheria/Wakili ambavyo ni vyeti vya kidato cha Nne au Sita kwa wale waliofika kiwango hicho na vyeti vya kuhitimu mafunzo mbalimbali kwa kuzingatia sifa za kazi husika Diploma/ Certificates, – Cheti cha Mitihani ya Kidato cha IV, VI, Computer Certificate, Vyeti vya Kitaaluma (Professional Certificate from Respective Boards).
- Testimonial “Provisional Result” Statement of Result “hati za matokeo ya kidato cha nne au cha sita (FORM IV AND FORM VI RESULTS SLIPS) HAZITAKUBALIWA.
- Waombaji wote waliosoma nje ya Nchi wahakikishe kuwa vyeti vyao vimehakikiwa na kuidhinishwa na mamlaka husika (TCU, NECTA na NACTE).
- Waombaji waliostafishwa katika Utumishi wa Umma hawaruhusiwi kuomba isipokuwa kama wana kibali kutoka kwa Katibu Mkuu Kiongozi.
- Waombaji wa kazi ambao tayari ni Waajiriwa katika nafasi za kuingilia walioko katika Utumishi wa Umma wasiombe na wanatakiwa kuzingatia maelekezo yaliyo katika Waraka Na. CAC.45/257/01/D/140 wa tarehe 30 Novemba, 2010.
- Uwasilishaji wa taarifa na sifa za kughushi wahusika kuchukuliwa hatua za kisheria.
- Mwisho wa kutuma maombi ya kazi ni tarehe 30/04/2025.
- MUHIMU: Kumbuka kuambatanisha barua yako ya maombi ya kazi iliyosainiwa pamoja na vyeti vya elimu, anuani ya barua hiyo ielekezwe kwa:
Mkurugenzi wa Manispaa,
Halmashauri ya Manispaa
S.L.P 318,
MOSHI-KILIMANJARO - Maombi yote yatumwe kwenye mfumo wa Kielekroniki wa Ajira (Recruitment Portal) kupitia anuani ya Ajira kwa kuingia sehemu iliyoandikwa “Recruitment Portal”.
- Maombi yatakayowasilishwa nje ya utaratibu uliowasilishwa katika tangazo hili HAYATAFIKIRIWA.
Imetolewa na: Mwajuma A. Nasombe
MKURUGENZI
HALMASHAURI YA MANISPAA MOSHI