Kila mwaka, baada ya matokeo ya Mtihani wa Taifa wa Kidato cha Nne kutangazwa, wanafunzi wengi nchini Tanzania husubiri kwa hamu kujua kama wamechaguliwa kujiunga na Kidato cha Tano au vyuo vya kati. Mchakato huu unaendeshwa na Ofisi ya Rais – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), ambayo inahusika na upangaji wa wanafunzi katika shule za sekondari za juu na vyuo vya kati kulingana na ufaulu wao na vigezo vingine vilivyowekwa.
Sifa na Vigezo Vinavyotumika kwenye Uchaguzi wa Wanafunzi
Katika mchakato wa kuchagua wanafunzi wa kujiunga na Kidato cha Tano na vyuo vya kati kwa mwaka 2025, TAMISEMI hutumia vigezo mbalimbali kuhakikisha uchaguzi unakuwa wa haki na unaozingatia sifa za wanafunzi. Vigezo hivi ni pamoja na:
- Ufaulu wa Masomo: Wanafunzi wanapaswa kuwa na alama za juu katika masomo yao ya msingi, hasa katika masomo yanayohusiana na tahasusi wanazotaka kusomea.
- Jumla ya Alama: Jumla ya alama katika masomo yote inazingatiwa, ambapo wanafunzi wenye alama za juu wana nafasi kubwa ya kuchaguliwa.
- Ufaulu katika Masomo ya Tahasusi: Wanafunzi wanapaswa kuwa na alama nzuri katika masomo yanayohusiana na tahasusi wanazotaka kusomea, kama vile PCM (Physics, Chemistry, Mathematics) au HGL (History, Geography, Language).
- Umri wa Mwanafunzi: Umri wa mwanafunzi pia unazingatiwa katika mchakato wa uchaguzi.
- Ushindani na Nafasi Shuleni: Nafasi zilizopo katika shule na ushindani kati ya wanafunzi huathiri uchaguzi.
- Wanafunzi wa Shule Binafsi au Nje ya Mfumo Rasmi: Wanafunzi waliomaliza katika shule binafsi au nje ya mfumo rasmi wanachaguliwa kwa kuzingatia ulinganifu wa matokeo yao kupitia Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA).
Tarehe ya Kutangazwa kwa majina ya Waliochaguliwa Kidato cha Tano
Kwa mujibu wa utaratibu wa miaka ya nyuma, TAMISEMI hutangaza majina ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Tano miezi michache baada ya matokeo ya Kidato cha Nne kutangazwa na NECTA. Kwa kawaida, majina haya hutolewa kuanzia mwishoni mwa mwezi Mei hadi katikati ya Juni. Kwa mfano: Mwaka 2019: Matokeo yalitangazwa Tarehe 01 June 2019, Mwaka 2020: Matokeo yalitangazwa Tarehe 17 June 2020, mwaka 2021: Matokeo yalitangazwa Juni 1, 2021, mwaka 2022: Matokeo yalitangazwa May 12, 2022, mwaka 2023: Matokeo yalitangazwa Juni 11, 2023 na mwaka 2024: Matokeo yalitangazwa Trehe 30 Mei 2024. Kwa mwaka huu wa 2025, inatarajiwa kwamba majina yatatangazwa kati ya Mei 31 hadi Juni 15, 2025.
Jinsi ya Kuangalia Majina ya Waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Tano
Kama mzazi au mwanafunzi, unaweza kufuatilia majina ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Tano mwaka 2025 kwa kupitia hatua zifuatazo:
Hatua ya 1: Kutembelea Tovuti Rasmi ya TAMISEMI ya Uchaguzi wa Wanafunzi wa Kidato cha Tano na Vyuo Vya Kati
- Tembelea tovuti rasmi ya TAMISEMI: https://selform.tamisemi.go.tz/content/selection-and-allocation/
- Bofya linki ya “Form Five First Selection, 2025”: Baada ya kufungua tovuti, tafuta na ubofye sehemu iliyoandikwa “Form Five First Selection, 2025”.
Hatua ya 2: Chagua Linki ya Mkoa Ulikosoma
- Orodha ya Mikoa: Baada ya kufungua linki ya “Form Five First Selection, 2025”, utakutana na orodha ya mikoa yote Tanzania.
- Chagua Mkoa: Tafuta na ubofye jina la mkoa ambao mwanafunzi alifanya mtihani wake wa Kidato cha Nne.
Hatua ya 3: Chagua Linki ya Halmashauri Ulikosoma
- Orodha ya Halmashauri: Baada ya kufungua linki ya mkoa husika, utaona orodha ya halmashauri zote ndani ya mkoa huo.
- Chagua Halmashauri: Tafuta na ubofye jina la halmashauri ambayo shule ya mwanafunzi ipo.
Hatua ya 4: Chagua Shule Uliyosoma
- Orodha ya Shule: Baada ya kufungua linki ya halmashauri husika, utaona orodha ya shule zote ndani ya halmashauri hiyo.
- Chagua Shule: Tafuta na ubofye jina la shule ambayo mwanafunzi alifanya mtihani wake wa Kidato cha Nne.
Hatua ya 5: Angalia Orodha ya Majina na Pakua Maelekezo ya Kujiunga (Joining Instructions)
- Orodha ya Majina: Baada ya kuchagua shule, utaona orodha ya majina ya wanafunzi waliochaguliwa pamoja na shule walizopangiwa.
- Pakua Joining Instructions: Unaweza kupakua maelekezo ya kujiunga (Joining Instructions) ya shule husika kwa kubofya linki ya jina la shule mbele ya namba na jina la mwanafunzi.
Hatua ya 6: Kuhakikisha Taarifa
- Thibitisha Taarifa: Hakikisha unachunguza majina kwa umakini ili kuthibitisha kama mwanafunzi amechaguliwa na wapi.
- Wasiliana na Ofisi za Elimu: Ikiwa kuna matatizo yoyote au maswali zaidi, unashauriwa kuwasiliana na ofisi za elimu za mkoa husika au kutumia namba za msaada zilizotolewa katika tovuti husika.
Majina ya Wanafunzi Waliochaguliwa Kidato cha Tano na Vyuo kwa Kila Mkoa
Hapa chini ni orodha ya linki za mikoa mbalimbali za kuangalia majina ya waliochaguliwa Kidato cha Tano 2025:
Mkoa |
Arusha |
Dar es Salaam |
Dodoma |
Geita |
Iringa |
Kagera |
Katavi |
Kigoma |
Kilimanjaro |
Lindi |
Manyara |
Mara |
Mbeya |
Morogoro |
Mtwara |
Mwanza |
Njombe |
Pwani |
Rukwa |
Ruvuma |
Shinyanga |
Simiyu |
Singida |
Songwe |
Tabora |
Tanga |
Hitimisho
Mchakato wa kuchagua wanafunzi kujiunga na Kidato cha Tano ni hatua muhimu katika mfumo wa elimu nchini Tanzania. Ni muhimu kwa wanafunzi na wazazi kufuatilia kwa karibu taarifa zinazotolewa na TAMISEMI na kuhakikisha wanazingatia taratibu zote zilizowekwa. Kwa kufuata hatua zilizoelezwa hapo juu, utaweza kuangalia majina ya waliochaguliwa na kufanya maandalizi muhimu kwa ajili ya kuanza masomo ya Kidato cha Tano.