Katibu wa Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma kwa niaba ya Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa anakaribisha Maombi ya kazi kutoka kwa Watanzania wenye sifa na uwezo wa kujaza nafasi 1,714 za ualimu kama ilivyoainishwa katika tangazo hili.
MWALIMU DARAJA LA III C – SOMO LA BIASHARA (BUSINESS STUDIES) NAFASI 700
- MAJUKUMU YA KAZI
- Kuandaa azimio la kazi, maandalio ya masomo, nukuu za masomo na Mpango wa Kazi wa majukumu mengine aliyokabidhiwa;
- Kutengeneza na Kufaraghua zana za kufundishia na kujifunzia;
- Kufundisha, kufanya Tathmini na kutunza kumbukumbu za Maendeleo ya Wanafunzi;
- Kusimamia na kufuatilia mahudhurio ya wanafunzi Shuleni na Darasani;
- Kusimamia malezi ya wanafunzi Kiakili, Kimwili, Kiroho na kutoa ushauri nasaha na unasihi;
- Kutoa ushauri wa Kitaalamu na kutaaluma kuhusu maendeleo ya
Elimu;
- Kusimamia na utunzaji wa vifaa na mali za Shule;
- Kazi nyingine atakazopangwa na Mkuu wa Shule kulingana na majukumu ya Shule
SIFA ZA MWOMBAJI
Kuajiriwa mwenye Shahada ya Elimu (Bachelor with Education) au Shahada ya Ualimu (Bachelor of Education) yenye somo la kufundishia la Biashara au Usimamizi wa Biashara (Commerce/ Bookkeeping/ Business Administration)
AU Shahada isiyo ya Ualimu/Elimu yenye somo la kufundishia la Biashara au usimamizi wa biashara (Commerce/ Bookkeeping/ Business Administration) pamoja na Stashahada ya Uzamili ya Elimu (Postgraduate Diploma in Education) kutoka Vyuo vya Elimu ya Juu vinavyotambulika na Serikali.
AU Wenye Shahada isiyo ya Ualimu katika fani ya Biashara/usimamizi wa biashara/Commerce/ Bookkeeping/ Business Administration/Business studies’’. waombaji ambao hawana somo la UALIMU ni lazima wawe tayari kupata mafunzo ya UALIMU baada ya kuajiriwa.
NGAZI YA MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali TGTS- D.
MWALIMU DARAJA LA III C – SOMO LA UCHUMI (ECONOMICS) NAFASI 850
- MAJUKUMU YA KAZI
- Kuandaa azimio la kazi, maandalio ya masomo, nukuu za masomo na Mpango wa Kazi wa majukumu mengine aliyokabidhiwa;
- Kutengeneza na Kufaraghua zana za kufundishia na kujifunzia;
- Kufundisha, kufanya Tathmini na kutunza kumbukumbu za Maendeleo ya Wanafunzi;
- Kusimamia na kufuatilia mahudhurio ya wanafunzi Shuleni na Darasani;
- Kusimamia malezi ya wanafunzi Kiakili, Kimwili, Kiroho na kutoa ushauri
nasaha na unasihi;
- Kutoa ushauri wa Kitaalamu na kutaaluma kuhusu maendeleo ya Elimu;
- Kusimamia na utunzaji wa vifaa na mali za Shule;
- Kazi nyingine atakazopangwa na Mkuu wa Shule kulingana na majukumu ya Shule
1.1.3 SIFA ZA MWOMBAJI
Kuajiriwa mwenye Shahada ya Elimu (Bachelor with Education) au Shahada ya Ualimu (Bachelor of Education) yenye somo la kufundishia la Uchumi (Economics)
AU Shahada isiyo ya Ualimu/Elimu yenye somo la kufundishia la Uchumi (Economics) pamoja na Stashahada ya Uzamili ya Elimu (Postgraduate Diploma in Education) kutoka Vyuo vya Elimu ya Juu vinavyotambulika na Serikali.
1.1.4 NGAZI YA MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali TGTS- D.
MWALIMU DARAJA LA III B – SOMO LA USHONAJI (DESIGNING, SEWING AND CLOTH TECHNOLOGY) NAFASI 2 –(LINARUDIWA)
- MAJUKUMU YA KAZI
- Kuandaa azimio la kazi, maandalio ya masomo, nukuu za masomo na Mpango wa Kazi wa majukumu mengine aliyokabidhiwa;
- Kutengeneza na Kufaragua zana za kufundishia na kujifunzia;
- Kufundisha, kufanya Tathimini na kutunza kumbukumbu za Maendeleo ya Wanafunzi;
- Kusimamia na kufuatilia mahudhurio ya wanafunzi Shuleni na Darasani;
- Kusimamia malezi ya wanafunzi Kiakili, Kimwili, Kiroho na kutoa ushauri nasaha na unasihi;
- Kutoa ushauri wa kitaalamu na kitaaluma kuhusu maendeleo ya Elimu;
- Kusimamia na utunzaji wa vifaa na mali za shule; na
- kazi nyingine atakazopangiwa na Mkuu wa Shule kulingana na majukumu
ya Shule.
1.1.6 SIFA ZA MWOMBAJI
Kuajiriwa mwenye cheti cha Mtihani wa Taifa wa Kidato cha Sita ambaye amefaulu masomo mawili au zaidi yanayofundishwa shuleni na kufaulu mafunzo ya Stashahada ya Ualimu ya miaka miwili (2) yenye somo la kufundishia la ushonsji au “Home Economics” kutoka Vyuo vya Ualimu vinavyotambulika na Serikali.
AU Wenye Stashahada isiyo ya Ualimu katika fani ya ushonaji au ‘’Home economicas’’. waombaji ambao hawana somo la UALIMU ni lazima wawe tayari kupata mafunzo ya UALIMU baada ya kuajiriwa.
1.1.7 NGAZI YA MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali TGTS- C.
MWALIMU DARAJA LA III B – SOMO LA HUDUMA YA CHAKULA VINYWAJI NA MAUZO (FOOD AND BEVARAGE, SALES AND SERVICES) NAFASI 22 – (LINARUDIWA)
- MAJUKUMU YA KAZI
- Kuandaa azimio la kazi, maandalio ya masomo, nukuu za masomo na Mpango wa Kazi wa majukumu mengine aliyokabidhiwa;
- Kutengeneza na Kufaragua zana za kufundishia na kujifunzia;
- Kufundisha, kufanya Tathimini na kutunza kumbukumbu za Maendeleo ya wanafunzi;
- Kusimamia na kufuatilia mahudhurio ya wanafunzi Shuleni na Darasani;
- Kusimamia malezi ya wanafunzi Kiakili, Kimwili, Kiroho na kutoa ushauri nasaha na unasihi;
- Kutoa ushauri wa kitaalamu na kitaaluma kuhusu maendeleo ya Elimu;
- Kusimamia na utunzaji wa vifaa na mali za shule; na
- Kazi nyingine atakazopangiwa na Mkuu wa Shule kulingana na majukumu ya Shule.
1.1.9 SIFA ZA MWOMBAJI
Kuajiriwa mwenye cheti cha Mtihani wa Taifa wa Kidato cha Sita ambaye amefaulu masomo mawili au zaidi yanayofundishwa shuleni na kufaulu mafunzo ya Stashahada ya Ualimu ya miaka miwili (2) yenye somo la kufundishia la somo la huduma ya chakula vinywaji na mauzo (Food and bevarage, sales and services) kutoka Vyuo vya Ualimu vinavyotambulika na Serikali.
AU Wenye Stashahada isiyo ya Ualimu katika fani ya Huduma ya Chakula, vinywaji na mauzo (Food and bevarage, sales and services). Waombaji ambao hawana somo la UALIMU ni lazima wawe tayari kupata mafunzo ya UALIMU baada ya kuajiriwa
1.1.10 NGAZI YA MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali TGTS- C.
MWALIMU DARAJA LA III B – SOMO LA UFUNGAJI WA NISHATI YA JUA (SOLAR POWER INSTALLATION) NAFASI 11 – (LINARUDIWA)
- MAJUKUMU YA KAZI
- Kuandaa azimio la kazi, maandalio ya masomo, nukuu za masomo na mpango wa Kazi wa majukumu mengine aliyokabidhiwa;
- Kutengeneza na Kufaragua zana za kufundishia na kujifunzia;
- Kufundisha, kufanya Tathimini na kutunza kumbukumbu za Maendeleo ya wanafunzi;
- Kusimamia na kufuatilia mahudhurio ya wanafunzi Shuleni na Darasani;
- Kusimamia malezi ya wanafunzi Kiakili, Kimwili, Kiroho na kutoa ushauri nasaha na unasihi;
- Kutoa ushauri wa kitaalamu na kitaaluma kuhusu maendeleo ya Elimu;
- Kusimamia na utunzaji wa vifaa na mali za shule; na
- Kazi nyingine atakazopangiwa na Mkuu wa Shule kulingana na majukumu
ya Shule.
1.1.12 SIFA ZA MWOMBAJI
Kuajiriwa mwenye Shahada ya Elimu (Bachelor with Education) au Shahada ya Ualimu (Bachelor of Education) yenye la Somo la Ufungaji wa Nishati ya Jua (Solar Power Installation au ‘’Power and Renewable Energy engineering’) kutoka katika vyuo vinavyotambuliwa na Serikali.
AU Shahada isiyo ya Ualimu/Elimu yenye somo la kufundishia la Somo la Ufungaji wa Nishati ya Jua (Solar Power Installation au ‘’Power and Renewable Energy engineering’’). Pamoja na Stashahada ya Uzamili ya Elimu (Postgraduate Diploma in Education) kutoka Vyuo vya Elimu ya Juu vinavyotambulika na Serikali.
AU Wenye Shahada isiyo ya Ualimu katika fani ya somo la kufundishia la Somo la Ufungaji wa Nishati ya Jua (Solar Power Installation au ‘’Power and Renewable Energy engineering’’). Waombaji ambao hawana somo la UALIMU ni lazima wawe tayari kupata mafunzo ya UALIMU baada ya kuajiriwa.
1.1.13 NGAZI YA MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali TGS- D.
MWALIMU DARAJA LA III B – SOMO LA (FOOD PRODUCTION) NAFASI 9 (LINARUDIWA)
- MAJUKUMU YA KAZI
- Kuandaa azimio la kazi, maandalio ya masomo, nukuu za masomo na Mpango wa Kazi wa majukumu mengine aliyokabidhiwa;
- Kutengeneza na Kufaragua zana za kufundishia na kujifunzia;
- Kufundisha, kufanya Tathimini na kutunza kumbukumbu za Maendeleo ya wanafunzi;
- Kusimamia na kufuatilia mahudhurio ya wanafunzi Shuleni na Darasani;
- Kusimamia malezi ya wanafunzi Kiakili, Kimwili, Kiroho na kutoa ushauri nasaha na unasihi;
- Kutoa ushauri wa kitaalamu na kitaaluma kuhusu maendeleo ya Elimu;
- Kusimamia na utunzaji wa vifaa na mali za shule; na
- Kazi nyingine atakazopangiwa na Mkuu wa Shule kulingana na majukumu ya Shule.
1.1.15 SIFA ZA MWOMBAJI
Kuajiriwa mwenye cheti cha Mtihani wa Taifa wa Kidato cha Sita ambaye amefaulu masomo mawili au zaidi yanayofundishwa shuleni na kufaulu mafunzo ya Stashahada ya Ualimu ya miaka miwili (2) yenye somo la kufundishia la Upishi (Food production) kutoka Vyuo vya Ualimu vinavyotambulika na Serikali.
AU Wenye Stashahada isiyo ya Ualimu katika fani ya Upishi (Food production). Waombaji ambao hawana somo la UALIMU ni lazima wawe tayari kupata mafunzo ya UALIMU baada ya kuajiriwa.
1.1.16 NGAZI YA MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali TGTS- C.
MWALIMU DARAJA LA III C – FIZIKIA (PHYSICS) – NAFASI 120
- MAJUKUMU YA KAZI
- Kuandaa azimio la kazi, maandalio ya masomo, nukuu za masomo na Mpango wa Kazi wa majukumu mengine aliyokabidhiwa;
- Kutengeneza na Kufaraghua zana za kufundishia na kujifunzia;
- Kufundisha, kufanya Tathmini na kutunza kumbukumbu za Maendeleo ya Wanafunzi;
- Kusimamia na kufuatilia mahudhurio ya wanafunzi Shuleni na Darasani;
- Kusimamia malezi ya wanafunzi Kiakili, Kimwili, Kiroho na kutoa ushauri nasaha na unasihi;
- Kutoa ushauri wa Kitaalamu na kutaaluma kuhusu maendeleo ya Elimu;
- Kusimamia na utunzaji wa vifaa na mali za Shule;
- Kazi nyingine atakazopangwa na Mkuu wa Shule kulingana na majukumu ya Shule.
1.1.18 SIFA ZA MWOMBAJI
Kuajiriwa mwenye Shahada ya Elimu (Bachelor with Education) au Shahada ya Ualimu (Bachelor of Education) yenye somo la kufundishia la Fizikia au Shahada isiyo ya Ualimu/Elimu yenye somo la kufundishia la Fizikia pamoja na Stashahada ya Uzamili ya Elimu (Postgraduate Diploma in Education) kutoka Vyuo vya Elimu ya Juu vinavyotambulika na Serikali
1.1.19 NGAZI YA MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali TGS- D.
AFISA KUMBUKUMBU II – NAFASI 10
- MAJUKUMU YA KAZIKudhibiti mifumo ya kumbukumbu, Kutunza na kusimamia matumizi ya kumbukumbu za Wizara, Idara zinazojitegemea, Vituo vya kutunzia kumbukumbu, Mikoa, Manispaa, Halmashauri za Wilaya, Nyaraka za Taifa na Mashirika ya Umma kulingana na mahali alipo;Kutambua na kutafuta kumbukumbu katika Masjala za Wizara, Mikoa, Idara Zinazojitegemea, Manispaa, Halmashauri za Wilaya na Vituo vya kuhifadhia Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa;Kudhibiti mfumo wa kumbukumbu zinazozalishwa na kompyuta, kutunza na kusimamia matumizi yake katika Wizara, Idara zinazojitegemea, Asasi na Serikali za Mitaa kulingana na mahali alipo; naKazi nyingine atakazopangiwa na Msimamizi wake wa kazi.
1.1.21 SIFA ZA MWOMBAJI
Kuajiriwa wenye Shahada ya kwanza katika fani ya Utunzaji na Uhifadhi wa Kumbukumbu (Records management and Archives) na nyingine zinazolingana nayo kutoka katika Vyuo vinavyotambuliwa na Serikali. Awe na ujuzi wa kutumia kompyuta.
1.1.22 NGAZI YA MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali TGS- D.
MASHARTI YA JUMLA.
- Waombaji wote wawe ni Raia wa Tanzania na wenye umri usiozidi miaka 45 isipokuwa kwa wale tu walioko kazini serikalini;
ii. Waombaji wa nafasi za Mwalimu Daraja la III B na Mwalimu Daraja la III C
wahakikishe wanambatisha HATI YA MATOKEO (ACADEMIC TRANSCRIPT) katika mfumo wa “Ajira Portal” kwa ajii ya utambuzi wa masomo ya kufundishia.
- Waombaji kazi wa kada ya Dereva II wenye leseni Daraja E au C wanapaswa KUAMBATISHA vyeti vya mafunzo ya Udereva vilivyowapatia sifa ya kupata madaraja husikaWaombaji wenye ulemavu wanahamasishwa kutuma maombi na wanapaswa kuainisha kwenye mfumo wa kuombea ajira ulemavu walionao kwa ajili ya taarifa kwa Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma;Waombaji wote waambatishe cheti cha kuzaliwa kilichothibitishwa na Mwanasheria/Wakili.Waombaji waambatishe maelezo binafsi yanayojitosheleza (Detailed C.V) yenye anwani na namba za simu za kuaminika pamoja na majina yawadhamini (referees) watatu wa kuaminika.Maombi yote yaambatane na vyeti vya taaluma, maelezo, nakala za vyeti vilivyothibitishwa na Mwanasheria/Wakili ambavyo ni vyeti vya kuzaliwa, kidato cha Nne, kidato cha Sita kwa wale waliofikia kiwango hicho, na vyeti vya kuhitimu mafunzo mbalimbali kwa kuzingatia sifa za kazi husika.
– Postgraduate/Degree/Advanced Diploma/Diploma/Certificates.
- Cheti cha mtihani wa kidato cha IV na VIComputer CertificateVyeti vya kitaaluma (Professional certificates from respective boards)“Testmonials”, “Provisional Results”, “Statement of results”, hati matokeo zakidato cha nne na sita (FORM IV AND FORM VI RESULTS SLIPS) HAVITAKUBALIWA.Waombaji waliosoma nje ya Tanzania wahakikishe vyeti vyao vimehakikiwa nakuidhinishwa na Mamlaka husika (TCU, NECTA na NACTE).Waombaji waliostaafishwa katika Utumishi wa Umma hawaruhusiwi kuomba isipokuwa kama wana kibali cha Katibu Mkuu Kiongozi.Waombaji kazi ambao tayari ni waajiriwa katika nafasi za kuingilia walioko katika Utumishi wa Umma wasiombe na wanatakiwa kuzingatia maelekezo yaliyo katika Waraka Na CAC. 45/257/01/D/140 wa tarehe 23 Novemba, 2010.Uwasilishaji wa taarifa na sifa za kughushi wahusika watachukuliwa hatua za KisheriaMwisho wa kutuma maombi ya kazi ni tarehe 14 Juni, 2025
MUHIMU: Kumbuka kuambatisha barua yako ya maombi ya kazi iliyosainiwa pamoja na vyeti vya elimu, anuani ya barua hiyo ielekezwe kwa; KATIBU, OFISI YA RAIS, SEKRETARIETI YA AJIRA KATIKA UTUMISHI WA UMMA, S. L. P. 2320, DODOMA.
- Maombi yote yatumwe kwenye mfumo wa kielektroniki wa Ajira (Recruitment Portal) kupitia anuani ifuatayo; http://portal.ajira.go.tz/ (Anuani hii pia inapatikana kwenye tovuti ya Sektretarieti ya Ajira kwa kuingia sehemu iliyoandikwa ‘Recruitment Portal’)
- Maombi yatakayowasilishwa nje ya utaratibu ulioainishwa katika tangazo hili HAYATAFIKIRIWA.
Limetolewa na;
KATIBU
SEKRETARIETI YA AJIRA KATIKA UTUMISHI WA UMMA.
pakua tangazo hapa; TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI MDAs NA LGAs 05-06-2025