Nafasi: Muuguzi wa Shule ya Msingi
Muhtasari wa Nafasi
Anaye ripoti kwa Mkuu wa Shule ya Sekondari na kufanya kazi kwa ukaribu na Naibu Mkuu Husika, Muuguzi wa Shule ya Sekondari atakuwa na jukumu la kutoa msaada wa kitabibu, afya na usalama kwa wanafunzi wa sekondari.
Sifa na Uzoefu Unaopendekezwa
- Uzoefu: Miaka 5+ ya uzoefu wa uuguzi katika huduma ya msingi na kushughulikia ajali za shule na uelewa wa majeraha.
- Lazima awe na Diploma ya Uuguzi. Shahada ya kwanza inapendelewa.
Ujuzi wa Kitaaluma:
- Uwezo mzuri wa mawasiliano kwa njia ya mazungumzo na maandishi
- Uwezo wa kusikiliza vizuri na kuelewa mahitaji na mitazamo ya wengine
- Uwezo wa kufanya maamuzi yenye busara, mwelekeo wa kutatua matatizo, uelewa wa ulinzi wa mtoto na afya na usalama
- Ujuzi mkubwa wa kujenga mahusiano na wadau mbalimbali
- Uwezo wa kufanya kazi kwa ukaribu na watoto, walimu na wafanyakazi wasio walimu kwa lengo la kutoa huduma bora kabisa.
Sifa Binafsi
- Mchezaji wa timu, msikilizaji mwenye huruma
- Uadilifu na uwezo wa kuweka siri
- Muwazo wa kimkakati, mwenye uwezo wa kubadilisha dira kuwa vitendo
- Ana mtazamo wa kimataifa, ana akili ya kihisia
- Kuelewa tamaduni mbalimbali, mbunifu, mwenye ushawishi
- Anayebadilika na mwenye uwezo wa kusimamia ukuaji na kuweka viwango vya juu
- Mzoefu wa mazingira ya lugha nyingi, mwenye msukumo, anayetangulia, mtaalamu na mlezi.
Majukumu
Majukumu ya msingi ya Muuguzi wa Shule ya Sekondari yatakuwa:
- Kupanga huduma ya kutunza watoto wakati wa wiki ya utambulisho wa wafanyakazi wapya
- Kutoa huduma ya kwanza, huduma za dharura, na matibabu inapohitajika
- Kuwajibika na matengenezo ya vifaa vya huduma ya kwanza katika Kampasi ya Sekondari
- Uwezo wa kufanya vipimo vya macho na masikio
- Kuweka kumbukumbu za mara kwa mara na sahihi za matatizo ya kiafya/afya za wanafunzi
- Kudumisha kumbukumbu zote za afya ya shule kwa usahihi, faragha, na usalama
- Kutoa dawa chini ya mwongozo uliowekwa na shule ya sekondari
- Kudumisha akiba ya dawa na vifaa vya huduma ya kwanza katika chumba cha muuguzi na kuhakikisha eneo hili linakuwa safi na nadhifu
- Kufanya majukumu mengine yoyote yatakayopewa na Mkuu wa Shule ya Sekondari
Maelezo ya Utafutaji
Mwombaji mtarajiwa wa nafasi ya Muuguzi anapaswa kuwa anapatikana Tanzania na aweze kuomba rasmi. Waombaji wanatakiwa kuwasilisha barua (kwa Kiingereza) inayoeleza uwezo wake na nia yake kwa nafasi hiyo, pamoja na wasifu wa sasa (CV). Majina, anuani na mawasiliano ya watu watatu (3) wa kumbukumbu. Maombi na maswali yaelekezwe kwa staffrecruitment@istafrica.com si zaidi ya Ijumaa tarehe 3 Mei, 2025 saa 9:00 alasiri.